Timu ya Agano la Krismasi imekuwa ikijishughulisha na kuhamazisha mashinani kwa muda wa miaka 3 iliyopita ambayo imepokelewa na kuungwa mkono kwa uwekaji kanda kutoka kwa Muungano wa Wamethodisti wengi. Kazi hii imezaa matunda kwa sababu taasisi na viongozi wa kanisa letu sasa wamekumbatia maadili na umuhimu wa kuweka kanda kwa mustakabali wa Kanisa la Muungano wa Methodisti.

Mnamo mwaka wa 2023, Timu ya Agano la Krismasi ilishirikiana na Kamati ya Kudumu ya maswala ya kanda za kati na Jedwali la Muungano ili kutoa sheria ya "Uenezaji wa majimbo Ulimwenguni" iliyowasilishwa kwa Kongamano kuu na Kamati ya Kudumu ya maswala ya kanda za kati

Uenezaji wa majimbo Ulimwenguni Pote ni toleo lililosasishwa la Agano la Krismasi. Timu ya Agano la Krismasi ilikubaliana kuungamkono mjadala wa Uenezaji wa majimbo Ulimwenguni.